Tashtiti: Matumizi katika Fasihi
Synopsis
Kitabu hiki kinabainisha namna watunzi wa fasihi hutumia tashtiti kutaja yasiyotajika bila kuchukiza, kuchukuliwa vibaya au kumwudhi msomaji. Tashtiti ni mbinu ya kuweka wazi na kurekebisha uovu na ujinga katika jamii kwa ucheshi. Tashtiti haiibui tu ucheshi bali ni ucheshi wenye lengo la kurekebisha. Nadharia Mfumo Tashtiti ya Highet inafafanua tashtiti kwa vipengele vyake kumi na moja ambavyo ndivyo huunda mfumo wa tashtiti. Vipengele hivi kumi na moja ni; kinaya, ukweli kinzani, mpomoko, tabaini, mwigo wa kubeza, usemi wa kimtaa, pujufu, vurugu, uangavu, chuku na mada za siku. Kitabu kinadhihirisha namna waandishi, kupitia kazi zao za fasihi, hufanyia mzaha mambo mazito wakiwa na lengo la kufichua uovu na ujinga katika jamii kwa ajili ya kuurekebisha. Kitabu hiki ni cha kipekee kwa namna kilivyosanifiwa. Mwandishi amepambanua tashtiti na vipengele vyake kwa njia ya wazi, ya kusisimua pamoja na mifano ya tungo za fasihi ambamo tashtiti imetumika. Utungo huu unapendekezewa wanafunzi wa fasihi katika vyuo vikuu, wahadhiri, watafiti na wadau wote katika elimu ya juu, mno wanataaluma wa Kiswahili.
Published
Categories
License

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License.
