Mofofonolojia Linganishi ya Lahaja za Kimaasai: Kenya na Tanzania

Authors

Alexander S. Meitamei

Synopsis

Mofofonolojia Linganishi ya Lahaja za Wamaasai – Kenya na Tanzania ni kazi ya kwanza kabisa kuchanganua lahaja za Kimaasai kwa misingi ya kisayansi. Ni kazi inayochanganua isimu ya lugha mojawapo ya Kiafrika na kufikia viwango vya kimataifa kama kazi zingine tajika za Katamba (1989), Lass (1984) na Mathews (1974). Lugha ya Kimaasai ina wingi wa lahaja zilizo na tofauti kimofofonolojia. Visawe vya nomino na vitenzi vimetambulishwa na sheria zinazosababisha utofauti kufafanuliwa kwa misingi ya mifanyiko ya kifonolojia na kimofolojia. Misingi ya nadharia mbalimbali za fonolojia na mofolojia zilitumika kama mwongozo wa uchanganuzi wenyewe. Kitabu hiki kitawafaa wanafunzi na walimu wa lugha ya Kiswahili hasa katika ngazi ya Vyuo vikuu. Pia kitawafaa Wanaisimu Kihistoria, wale wanaoshughulikia elimu lahaja na wale wanaonuiwa kujifunza lugha ya Kimaasai. Ni nyongeza kwa tafiti chache za kiisimu za lugha za Nilo-Sahara zilizopo.

Utafiti Academic Press

Published

2020

Categories